Jumapili 17 Mei 2026 - 12:00
Watawala vibaraka wa eneo hili wachukue funzo kutokana na hatima ya Saddam/ Subira ya Iran inakaribia kuisha

Hawza/ Mjumbe wa kamati ya uongozi ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi aliwaonya watawala vibaraka wa eneo hili kwa kusema: Sisi tutawapa tena fursa ndogo, ihesabuni kuwa ni neema, siku ipo karibu ambapo tawala zenu zitaondolewa, siku hiyo Marekani haitawaokoa tena, ikiwa Marekani italeta meli zake za kivita karibu nanyi, itapigwa pigo ambalo haitaweza tena kuinuka.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Mohsen Araki, usiku uliopita katika mkusanyiko mkubwa wa wanazuoni wa Hawza na Umma wa Hizbullah kwa ajili ya kuwaunga mkono Mashia waliodhulumiwa wa eneo hili (Bahrain, Kuwait, Imarati na kadhalika), uliofanyika katika ukumbi wa Imam Khomeini (r.a) ndani ya Haram tukufu ya Hadhrat Ma’sumah (a.s), alizungumzia sunna za Mwenyezi Mungu zinazotawala jamii za wanadamu na akachambua hali ya sasa ya eneo hili na dunia.

Mjumbe wa Baraza Kuu la Hawza mwanzoni mwa hotuba yake, huku akisisitiza sunna za Mwenyezi Mungu, alisema: Yale yanayotokea leo katika eneo letu ni sehemu ya sunna za Mwenyezi Mungu ambazo Mwenyezi Mungu Mtukufu amezitaja ndani ya Qur’ani na ametufahamisha jukumu letu ndani ya mfumo wa sunna hizi, kila kinachotokea katika jamii za wanadamu kinafanyika kwa mujibu wa sheria na sunna ya Mwenyezi Mungu, kama ambavyo maumbile na ulimwengu wa uumbaji vinafanya kazi kwa msingi wa sheria.

Mjumbe wa kamati ya uongozi ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi aliongeza: Sunna za kijamii zilizotajwa katika Qur’ani Tukufu na katika riwaya za Maasumu (a.s) zinaweza kugawanywa katika makundi matatu.

Mjumbe wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Qum akifafanua kundi la kwanza la sunna za Mwenyezi Mungu alisema: Kundi la kwanza ni sunna zinazotawala mwenendo wa viongozi wa kimungu. Mojawapo ya sunna muhimu zaidi ni “sunna ya kuwepo na ghaiba”, asili ya kuwepo kwa kiongozi wa kimungu katika jamii ya wanadamu ni irada ya Mwenyezi Mungu isiyoweza kubadilika, kwa mujibu wa sunna ya Mwenyezi Mungu, katika kila jamii na kila zama, lazima kuwe na kiongozi aliyeteuliwa na Mwenyezi Mungu.

Ayatullah Araki aliendelea: Aina tatu za ghaiba kwa viongozi wa kimungu zimekuja katika Aya na riwaya: ghaiba ya mahali (kama hijra ya Mtume Mtukufu (s.a.w.w) kutoka Makka kwenda Madina na hijra ya Nabii Ibrahim (a.s) kutoka Babel kwenda Palestina), ghaiba ya kusimamishwa jukumu (kusimamishwa jukumu la jihadi kutoka kwa Maimamu wa uongofu (a.s) baada ya Sayyidush-Shuhada (a.s) mpaka kudhihiri kwa Imam wa Zama (a.f)) na ghaiba ya wakati (ghaiba ya Hadhrat Walii wa zama (a.f)).

Mjumbe wa Baraza Kuu la Hawza za Kielimu aliendelea kwa kuashiria kundi la pili la sunna za Mwenyezi Mungu na kusema: Kundi la pili ni sunna zinazotawala jamii za Kiimani; jamii ambazo huungana na viongozi wa kimungu kupitia “agano la utiifu” na “agano la nusura”. Jamii ya Kiimani ni jamii ambayo ndani ya mfumo wa maagano haya mawili hujifanya mfuasi wa viongozi wa kimungu, ikiwa jamii ya Kiimani itatimiza ahadi yake, itafikia heshima, nguvu, ustawi na ubora.

Akirejelea hatima ya Bani Israil alisema: Bani Israil walikuwa wakitekeleza maagano haya mawili, lakini baada ya kuvunja agano walipatwa na matatizo, kwa masikitiko, uvunjaji huu wa agano ulitokea pia katika jamii ya Kiislamu baada ya kufariki kwa Mtume Mtukufu (s.a.w.w), na ulijaribiwa katika hatua tatu pamoja na Amirul-Muuminin (a.s), Imam Mujtaba (a.s) na Sayyidush-Shuhada (a.s), ambapo kilele chake kilikuwa Karbala.

Jamhuri ya Kiislamu; nembo ya kurejea katika agano

Mjumbe wa kamati ya uongozi ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi alisisitiza kuws: Jamhuri ya Kiislamu ni nembo ya kurejea katika agano hili.

Watu ambao leo wanakusanyika barabarani wanatangaza kuwa: “Tutatoa maisha yetu lakini hatutakubali fedheha.” Walituua, wakaharibu nyumba zetu, wakatupiga mabomu kwa siku arobaini mfululizo, lakini taifa hili halikuacha utiifu kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na nusura kwa Walii wa Mwenyezi Mungu.

Mjumbe wa Baraza la Kutambua Maslahi ya Mfumo, akirejelea Aya tukufu: وَكانَ حَقًّا عَلَينا نَصرُ المُؤمِنينَ aliongeza kusema: Kurejea huku bila shaka kutaambatana na nusura ya Mwenyezi Mungu, tuna yakini kuwa ushindi mkubwa utapatikana katika taifa la Iran.

Ayatullah Araki aliendelea kuelezea kundi la tatu la sunna za Mwenyezi Mungu na kusema: Kundi la tatu ni sunna zinazohusiana na watawala na matwaghuti wanaotawala jamii za wanadamu, sunna mbili muhimu ndani ya Qur’ani zinawatawala hawa: “sunna ya kupewa muhula” na “sunna ya kushikwa”. Mwenyezi Mungu huwapa matwaghuti muhula ili wafanye kila wawezalo, huyu Trump anasema yale yale aliyosema Firauni: أَنا رَبُّكُمُ الأَعلَى Lakini hatua kwa hatua kuna dalili kwamba Mwenyezi Mungu ameacha sunna ya kupewa muhula na sasa imefika zamu ya sunna ya kushikwa.

Mwalimu wa darsa za wazi ndani ya Hawza ya Qum, huku akifafanua sunna ya kushikwa ya Mwenyezi Mungu alisema: Katika sunna ya kushikwa, Mwenyezi Mungu huanza kuwabana matwaghuti hatua kwa hatua mpaka kuwaangamiza kabisa. Mara nyingi mkondo huu huanza kutoka kwa matwaghuti wenyewe, Mwenyezi Mungu alimwangamiza Saddam Baath kwa mikono yake mwenyewe, leo Trump kwa mikono yake mwenyewe anajitumbukiza shimoni, hii ina maana kuwa sunna ya kushikwa kwa Marekani imewadia.

Kwa nini hamchukui funzo kutoka kwa Saddam?

Mjumbe wa kamati ya uongozi ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi akiwaambia watawala wa Kuwait, Bahrain, Imarati na Saudi Arabia alisema: Kwa nini hamchukui funzo kutoka kwa Saddam? Saddam alikuwa na nguvu zaidi kuliko nyinyi nyote, na uungaji mkono wa Marekani kwa Saddam haukuwa mdogo kuliko ule wa kwenu, Mwenyezi Mungu aliitekeleza sunna hii kwa Saddam mara moja, na sasa imefika zamu yenu.

Mjumbe wa Baraza la Kutambua Maslahi ya Mfumo aliongeza: Kwa miaka hamsini mmekuwa mkifanya jinai dhidi ya Iran na Mashia, Saudi Arabia imewaua wanazuoni wangapi wa Kishia? Ninyi wa Imarati mmefanya jinai kiasi gani Yemen, Libya na Sudan? Sasa imefika zamu yenu.

Ayatullah Araki huku akisisitiza nguvu ya sasa ya Mashia alisema: Leo Mashia wa Iran, Iraq, Lebanon, Yemen na maeneo ya kusini mwa Ghuba ya Uajemi ni nguvu kubwa zaidi katika eneo hili, si Marekani wala nyinyi, leo mnaona mkono wa juu wa Jamhuri ya Kiislamu.

Trump alienda China kwa udhalili na akarudi kwa fedheha

Mjumbe wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Qum, akirejelea safari ya hivi karibuni ya Trump kwenda China alisema: Trump alienda China kwa udhalili, akapigwa kibao cha fedheha na akarudi, Mwenyezi Mungu Mtukufu ameonesha tukio hili ili kuwaonesha wote kuwa anamfedhehesha hatua kwa hatua.

Onyo kwa viongozi vibaraka na mamluki wa eneo hili

Mjumbe wa kamati ya uongozi ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi akiwaonya watawala vibaraka wa eneo hili alisema: Sisi tutawapa tena fursa ndogo, ihesabuni kuwa ni neema, siku iko karibu ambapo tawala zenu zitaondolewa, siku hiyo Marekani haitawaokoa tena, Ikiwa Marekani italeta meli zake za kivita karibu nanyi, itapigwa pigo ambalo haitaweza tena kuinuka.

Ayatullah Araki alisema: Jamhuri ya Kiislamu na nguvu zote za muqawama za eneo hili zimevumilia, hakujabaki mengi katika subira hii, kipimo hiki kikifurika, hakuna kitakachobaki kwenu, acheni kuwadhulumu Mashia, wanazuoni wa Kishia wa Bahrain, Saudi Arabia na maeneo mengine wako katika magereza yenu, maelfu ya Wairani wamefungwa huko Imarati, inawezekana kweli sisi tuvumilie na kunyamaza?

Mjumbe wa Baraza Kuu la Hawza mwishoni, kwa kutawassal kwa Hadhrat Walii wa zama (a.f), alisema: Tunamwambia Hadhrat Walii wa zama (a.f): Ewe mtukufu! Kwa mkono wako taifa letu limepiga hatua mbele, kwa mkono wako nchi hii imeendeshwa, tumeuona waziwazi mkono wa Imam wa zama katika matukio, hususan baada ya shahada ya kiongozi wetu mpendwa na kipenzi chetu.

Ewe Mwenyezi Mungu! Kijaze kipimo hiki na uikamilishe nusura yetu, na uiondoe shari ya maadui wetu katika eneo hili.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha